Taarifa mpya kutoka Simba Leo Jumanne - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa mpya kutoka Simba Leo Jumanne

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema wiki hii watakamilisha zoezi la kuagana na wachezaji ambao hawataendelea nao msimu ujao


Ahmed amesema klabu bado iko kwenye mazungumzo na baadhi ya wachezaji ambao wengine watawasitishia mikataba yao kwa kuwa hawamo katika mipango ya Kocha Robertiho Oliveira katika msimu ujao


"Bado hatujafunga zoezi la kuagana na baadhi ya wachezaji, tuko kwenye mazungumzo ya kusitisha mikataba ya wachezaji ambao hawatakuwa nasi msimu ujao"


"Tunatarajia zoezi hili tutalikamilisha wiki hii ili wiki ijayo tuanze kutambulisha wachezaji tuliowasajili kuchukua nafasi za wachezaji walioachwa," alisema Ahmed


Wachezaji ambao mpaka sasa wamepewa mkono wa kwaheri na klabu ya Simba ni Augustine Okrah, Victor Akpan, Nelson Okwa na Mohammed Ouattara


Wengine ni Beno Kakolanya, Erasto Nyoni na Jonas Mkude



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz