Mgunda: Chama na Kanoute hatutakuwa nao - EDUSPORTSTZ

Latest

Mgunda: Chama na Kanoute hatutakuwa nao

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Kuelekea Mechi ya Ligi Kuu Ya NBC Simba Sc dhidi ya Polisi Tanzania kesho katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Kocha Msaidizi wa Simba Sc Juma Mgunda ameelezea maandalizi yao yalivyo mpaka sasa.


Mgunda ameesema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari kuelekea mchezo huo huku akitaja mastaa watakaoukosa mchezo huo.


"Maandalizi yote ya kucheza na timu nzuri ya Polisi hapo kesho yamekamilika. Huu ni mchezo muhimu wa Ligi na ni muhimu kwetu. Ilituonekane tumeshiriki vizuri ligi lazima tuucheze.


"Sisi tumejipanga kwa sababu tunajua ni muhimu ili kumaliza ligi vizuri. Ni mechi ambayo ina umhimu wa kipekee.


"Wachezaji ambao tutawakosa ni Chama kwa sababu ana adhabu ya TFF ya kutocheza mechi tatu za ligi, pia tutamkosa Sadio Kanoute ambaye naye ana kadi tatu za njano na ameondoka kikosini yupo nchini kwao, waliobaki wote wapo tayari kuitumikia Simba kesho," amesema Mgunda.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz