KMC yabaki Ligi Kuu, yaichapa Mbeya City - EDUSPORTSTZ

Latest

KMC yabaki Ligi Kuu, yaichapa Mbeya City

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Ni KMC ambao wamefanikiwa kubaki Ligi Kuu msimu ujao kwa kuwafunga Mbeya City kipigo cha mabao 2-0 ikiwa ni mchezo wa marudiano uliofanyika katika uwanja wa Uhuru.


Mabao yote yalipatikana katika kipindi cha kwanza bao lilofungua dimba likipatikana dakika ya tatu lililofungwa na Daruweshi Saliboko na kumaliziwa dakika 27 na Aweso Aweso.


KMC walipishana kwa alama moja katika msimamo wa Ligi huku watoto wa Kinondoni wakiwa na pointi 32 na Mbeya City kuwa na pointi 31.


Mbeya City imebakiza nafasi moja ya lala salama watakapokutana na Mashujaa kucheza play off itakayoamua safari yao ya kubaki Ligi Kuu msimu ujao.


Mchezo huo wa muhimu kwa pande zote mbili utafanyika tarehe 19 katika uwanja wa Lake Tanganyika na marudiano yatamalizika tarehe 24 June uwanja wa Sokoine Mbeya.


Huku Mashujaa wanapigania kupanda Ligi Kuu na Mbeya City wakitamani kusalia kundini.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz