Ahmed Ally akoleza Saido kuchukua kiatu cha dhahabu ligi kuu - EDUSPORTSTZ

Latest

Ahmed Ally akoleza Saido kuchukua kiatu cha dhahabu ligi kuu

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Baada ya kiungo wa Simba, Saido Ntibazonkiza kumsogelea kwa ufungaji mshambuliaji Fiston Mayele wa Yanga mwenye mabao 16 na yeye 15, uongozi wa Simba umetoa neno.


Simba jana Juni 6 ilishinda mabao 6-1 huku Saido akiweka wavuni mabao 5 akipaa kutoka 10 hadi 15.


Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema wanakitaka kiatu cha ufungaji bora msimu wa 2022/23 na mechi ya mwisho ya msimu watamsaidia Saido ili akibebe.


Ligi Kuu Bara imebaki mechi moja kutamatakika ambapo Simba itacheza dhidi ya Coastal Union Dar na Yanga itacheza dhidi ya Tanzania Prisons Sumbawanga.


"Tunahitaji mfungaji bora, zimesalia bao 2 na hakuna mashaka kwenye mechi ya mwisho ya Coastal tutamsaidia timu nzima awe mfungaji bora," amesema Ahmed na kuongeza;


"Uliona kuna nafasi John Bocco alikuwa nafasi ya kufunga akasema hii ya Saido akamwekea akafunga, bao la tano alikuwa na uwezo wa kufunga Kibu lakini akamtengea Saido,"


Chanzo: Mwanaspoti



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz