Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
Yanga inaweza kwenda Afrika Kusini ikiwa tayari imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC kama itapata ushindi katika mchezo dhidi ya Dodoma Jiji
Hili ni jambo muhimu kwa Wananchi kuhakikisha linakamilika ili kuwekeza nguvu katika mechi mbili zitakazofuata
May 17 Yanga itacheza na mchezo wa marudiano dhidi ya Marumo Gallants katika uwanja wa The Royal Bafokeng huko Afrika Kusini
Baada ya mchezo huo Wananchi watarejea Tanzania kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Singida BS ambao utapigwa May 21 katika uwanja wa LITI, Singida
Yanga ina dakika 270 za kuweka rekodi ya aina yake kwenye soka la Tanzania ambazo ni kutwaa taji la Ligi Kuu kwa mara ya 29, kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika na pia kutinga fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC)
Zaidi Yanga inawania rekodi ya kushinda mataji manne msimu huu Ngao ya Jamii (tayari), Ligi Kuu, CAF CC na ASFC
No comments:
Post a Comment