MATCHDAY: YANGA VS MARUMO GALLANTS Itazame hapa - EDUSPORTSTZ

Latest

MATCHDAY: YANGA VS MARUMO GALLANTS Itazame hapa

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Historia inakwenda kuandikwa uwanja wa Benjamin Mkapa leo ambapo utashuhudiwa mchezo wa nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika kati ya Yanga dhidi ya Marumo Gallants


Ni kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Benjamin Mkapa timu ya Tanzania itacheza mechi ya nusu fainali katika mashindano ya CAF ngazi ya klabu


Utakuwa mchezo muhimu kwa Yanga kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga fainali wakati timu hizo zitakaporudiana wiki ijayo huko Afrika Kusini


Kwa mashabiki wa soka nchini hii ni fursa adimu, kushuhudia mchezo wa nusu fainali mashindano ya CAF katika ardhi ya Tanzania


Kwa wale ambao bado hawajapata tiketi wanayo nafasi ya kununua tiketi kwani bado mauzo ya tiketi hayajafungwa


Tiketi za VIP A zimemalizika hivyo tiketi zinazopatikana ni VIP B, C na Mzunguuko


Jana wakati anazungumza na Wanahabari, Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi aliwataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa kuishangilia timu yao


Nabi alisema nguvu ya mashabiki iliwasaidia kufanya vizuri katika mechi zote walizocheza nyumbani katika mashindano hayo msimu huu sasa wanawahitaji kwa wingi zaidi leo katika mechi muhimu ya kusaka tiketi ya kutinga fainali


Alibainisha kuwa wachezaji wake wote wako tayari kwa mchezo huo utakaopigwa kuanzia saa 10 jioniPia mechi itakuwa LIVE kwenye app yetu bofya hapa kuidownload sasa



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz