Mandonga kuzichapa na Mmalawi dodoma - EDUSPORTSTZ

Latest

Mandonga kuzichapa na Mmalawi dodoma

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Bondia Karim Mandonga anatarajia kupanda ulingoni dhidi ya Alick Mwenda wa Malawi katika pambano linalotarajia kupigwa Juni 24, mwaka huu kwenye Viwanja vya Chinangale mkoani Dodoma.


Mandonga anapanda ulingoni kwenye pambano hilo ikiwa ni miezi miwili tangu amchape Kenneth Lukyamuzi wa Uganda nchini Kenya katika pambano la kuwania mkanda wa Ubingwa wa PST Afrika Mashariki na Kati.


Mandonga amesema kuwa anatarajia kurejea ulingoni kuzichapa dhidi ya Mwenda wa Malawi katika pambano ambalo litakalopigwa kwa raundi nane.


“Nashukuru Mungu nipo sawa natarajia kurejea ulingoni Juni 24, mwaka huu pale Dodoma, hii kwangu itakuwa ni mara ya kwanza kupigana ndani ya Jiji la Dodoma Mandonga Mtu Kazi, niwaambie mashabiki wangu nakuja huko kufanya maajabu.”


“Huyo Mwenda anatakiwa ajiandae kweli kwa sababu tayari nimeshaingia kambini kwa ajili ya pambano hilo, anatakiwa kujua nishapiga watu nje na kuipa sifa kubwa Tanzania basi na yeye nitampiga na kuendelea kuipa sifa nchini yangu katika pambano langu hilo,” amesema Mandonga.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz