Man United hali tete, wachezea kichapo kwa West Ham - EDUSPORTSTZ

Latest

Man United hali tete, wachezea kichapo kwa West Ham

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Wenyeji West Ham United wameibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Jumapili Uwanja wa London.


Bao pekee la West Ham United limefungwa na mshambuliaji Mualgeria, Mohamed Saïd Benrahma aliyemtungua kipa David de Gea kwa shuti la umbali wa mita 20 dakika ya 27.


Kwa ushindi huo, West Ham United ya kocha David Moyes inafikisha pointi 37 katika mchezo wa 35, ingawa inabaki nafasi ya 15, wakati Manchester United inabaki na pointi zake 63 za mechi 34 nafasi ya nne.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz