Kamati yakamilisha uchunguzi kuzimika kwa taa Dimba la Mkapa - EDUSPORTSTZ

Latest

Kamati yakamilisha uchunguzi kuzimika kwa taa Dimba la Mkapa

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana jana May 06, 2023 akiwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, amepokea taarifa ya Kamati aliyoiunda kuchunguza tukio la kukatika umeme katika uwanja huo wakati wa mechi ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika kati Timu ya Yanga na Rivers United ya Nigeria.


Baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri Dkt. Chana amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Said Yakubu kufanyia kazi taarifa hiyo ikiwemo kuchukua hatua zinazostahili kulingana na taarifa hiyo ambapo tukio hilo la kupokea taarifa limehudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu, Nicholaus Mkapa.


Kamati hiyo imeongozwa na Mwenyekiti Mhandisi Keneth Boymanda kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), ikiwa na Wajumbe kutoka Wakala wa Majengo (TBA) na baadhi ya Watumishi wa Wizara.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz