Yanga kuwafuata Rivers United siku hii - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga kuwafuata Rivers United siku hii

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kikosi cha Yanga kitaondoka nchini Alhamisi kuelekea Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Rivers United


Mchezo huo utapigwa Jumapili, April 23 huko Nigeria katika uwanja wa Godswill Akpabio uliopo mji wa Uyo


Rivers United walitumia uwanja huo kwenye hatua ya makundi na baadae wakaomba kuruhusiwa kurejea kwenye uwanja wao wa Adokiye Amiesimaka huko Port Harcort ila Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limegomea mabadiliko hayo baada ya kufanyia ukaguzi uwanja huo na kubaini bado haukidhi vigezo


Yanga inasaka nafasi ya kutinga nusu fainali ya michuano hiyo, itahitaji ushindi au hata matokeo ya sare ugenini kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa jijini Dar es salaam


Mchezo wa marudiano utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, April 30 2023



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz