USAJILI: Nyota yamuwakia vizuri beki wa Yanga Bacca - EDUSPORTSTZ

Latest

USAJILI: Nyota yamuwakia vizuri beki wa Yanga Bacca

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Baada ya kuridhishwa na kiwango chake, klabu ya Yanga iko mbioni kumuongeza mkataba beki Ibrahim Bacca


Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema tayari mazungumzo yameanza wakilenga kumuongeza mkataba pamoja na kuboresha maslahi yake


"Tutafanya jambo kubwa kwa Bacca tushaanza mazungumzo nae, amefanya vizuri lazima tumuongezee, tumpe malipo mazuri zaidi, duniani kote ipo hivyo ukifanya vizuri unaongezewa na usipofanya vizuri mkataba wako ukiisha utapewa nafasi ya kuondoka," alisema Hersi


Bacca alikuwa sehemu ya kikosi kilichopata ushindi dhidi ya Rivers United nchini Nigeria katika mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali kombe la Shirikisho barani Afrika


Kiwango chake kimeimarika na sasa ameanza kujihakikishia nafasi kwenye kikosi cha kwanza



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz