Umemsikia kocha wa Simba alivyowatambia Watani zake Yanga?? - EDUSPORTSTZ

Latest

Umemsikia kocha wa Simba alivyowatambia Watani zake Yanga??

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mechi ya Kariakoo Dabi Aprili 16 itakuwa ni ya kwanza kwa Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira, mwenyewe amesema anaisubiri mechi hiyo kwa hamu


Wakati akiinoa Vipers Fc, Robertinho amewahi kukutana na Yanga katika mechi ya kirafiki katika kilele cha Wiki ya Mwananchi na kubuka na ushindi wa mabao 2-0


Robertinho amesema anatambua ukubwa wa mechi ya dabi inayozikutanisha Simba na Yanga, lakini kamwe hawezi kuingia presha ya mchezo huo na kwamba anausubiri kwa hamu ili timu yake ionyeshe ubora walionao


"Presha juu ya Yanga? Hapana siwezi kuwa na hali hiyo kabisa kwanza mimi napenda mechi kama hizi ambazo mashabiki wanajaa uwanjani na kuwa na msisimkjo mkubwa"


"Nimeshashinda mechi kubwa katika Uwanja kama Mracana kule kwetu Brazil ukiwa umejaa," alisema Robertinho


"Tunaiheshimu Yanga lakini hata sisi tunaitaka hii mechi ili tuthibitishe ubora wetu mbele ya mashabiki wetu jambo zuri imekaa sehemu nzuri kwani kama tukishinda basi tutakuwa tumefanya maandalizi mazuri na kuongeza morali kuelekea mechi ijayo ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Wydad Casablanca"



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz