Tetesi za usajili ndani ya klabu ya Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

Tetesi za usajili ndani ya klabu ya Yanga

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kuelekea mchezo dhidi ya Simba siku ya Jumapili, zilianza kuibuka tetesi kuwa klabu hiyo inamvizia beki wa kati wa Yanga Dickson Job ambaye kimsingi tayari alikuwa amefikia makubaliano ya kuongeza mkataba kuendelea kuwatumikia Wananchi


Imeelezwa Yanga imefunga mjadala na Job baada ya mchezaji huyo kusaini mkataba wa miaka miwili


Mkataba wake wa awali ulikuwa unamalizika mwishoni mwa msimu lakini sasa ni uhakika ataendelea kubaki na Yanga kwa miaka mingine miwili


Yanga imeendelea kuhuisha mikataba ya nyota wake ambao mwishoni mwa msimu watakuwa huru ili kuepuka mresha ya kusubiri mpaka mikataba yao ifikie tamati


Djigui Diarra, Yannick Bangala, Djuma Shabani, Mudathir Yahya, Bakari Nondo Mwamnyeto, Fiston Mayele, Farid Mussa, Zawadi Mauya ni miongoni mwa wachezaji ambao tayari mikataba yao imehuishwa



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz