Tetesi za usajili barani ulaya Leo Ijumaa - EDUSPORTSTZ

Latest

Tetesi za usajili barani ulaya Leo Ijumaa

 

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Chelsea imewasiliana na meneja wa zamani na mkufunzi wa sasa wa Roma Jose Mourinho kuhusu kurejea kwake kwa mara ya tatu katika klabu hiyo ya Stamford Bridge. (Relevo – In Hispanic)


Mourinho pia amepokea ofa ya euro 120m (£105m) kufunza Saudi Arabia kwa miaka miwili. (Corriere dello Sport - kwa Kiitaliano)


Chelsea wanatazamia kutaka kumnunua mshambuliaji wa Benfica wa Ureno Goncalo Ramos, 21. (Football Insider)


Inter Milan wanataka kumfunga beki wa kati wa Italia Alessandro Bastoni, 23, ili aongeze kandarasi mpya huku Manchester City ikimnyatia. (Calciomercato – In Italic)


Tottenham wamemchukua beki wa Scotland Ben Brannan, 16, kwa majaribio kutoka Kilmarnock kabla ya uwezekano wa kuhama. (Football Insider)


Barcelona wana imani wanaweza kumsajili beki wa pembeni wa Ureno Joao Cancelo kutoka Manchester City msimu huu wa joto. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 kwa sasa yuko kwa mkopo Bayern Munich. (Sport – In Hispanic )


Manchester United wamekuwa kwenye mazungumzo kwa wiki kadhaa kuhusu kumsajili Jeremie Frimpong kutoka Bayer Leverkusen, ambaye atahitaji euro 50m (£43.9m). (Bild - in German).


Barcelona na Bayern Munich wamefuata Manchester United ili kutaka kukutana na wakala wa Frimpong kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kuhama kutoka Bayer Leverkusen msimu huu wa joto. (Fabrizio Romano)


AC Milan wamefikia makubaliano na Rafael Leao kuhusu mkataba mpya na mshambuliaji huyo wa Ureno, 23. (Relevo - in Spanish)


Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, anaangaziwa sana katika video ya Paris St-Germain ili kutangaza uboreshaji wa tikiti za msimu wa 2023-24 lakini Lionel Messi wa Argentina, 35, au mshambuliaji wa Brazil Neymar, 31 hawajatajwa. (Le Parisien - in Kifaransa)


Kiungo wa kati wa Austria Marcel Sabitzer, 29, atafikiria kufanya uhamisho wake wa mkopo kutoka Bayern Munich hadi Manchester United kuwa mkataba wa kudumu. (Sky Sport)


Arsenal wanaongeza juhudi zao za kumsajili kiungo wa kati wa Uswizi Djibril Sow, 26, kutoka Eintracht Frankfurt msimu wa joto. (mail)


Winga wa West Ham na England Jarrod Bowen, 26, anasakwa na Newcastle. (Sport) Leeds United itatafuta kumsajili kiungo wa kati wa Marekani anayecheza kwa mkopo Weston McKennie, 24, kutoka Juventus kwa kudumu iwapo wataepuka kushushwa daraja kutoka kwa Ligi ya Premia. (Calciomercato – In Italia)


Klabu ya Uturuki Altay SK inasema kuwa Manchester City, Atletico Madrid na Sevilla wametoa ofa kwa ajili ya mlinzi wao wa Uturuki Efe Sarikaya, 17. (Sport - in Spanish)


Leeds United sasa wanaongoza Everton katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Coventry City na Uswidi Viktor Gyokeres, 24, msimu huu wa joto. (Football Insider)


Mshambulizi wa Valencia na Uruguay Edinson Cavani, 36, anasema hafikirii kustaafu. (AS – In Hispanic)


BBC



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz