Ten Hag achekelea kurudi Kwa Eriksen kikosini - EDUSPORTSTZ

Latest

Ten Hag achekelea kurudi Kwa Eriksen kikosini

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Meneja wa Manchester United Erik ten Hag alisema alihofia Christian Eriksen atakosa msimu uliosalia baada ya kuumia kifundo cha mguu katika mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Reading mwezi Januari


Eriksen anarejea kwenye kikosi cha United kwa ajili ya mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu dhidi ya Everton kwenye Uwanja wa Old Trafford


Ten Hag ana furaha kiungo huyo wa Denmark amerejea kabla ya muda uliopangwa


Hata hivyo, bado amekasirishwa na jinsi jeraha hilo lilivyosababishwa na rafu kutoka kwa Andy Carroll


Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Newcastle hakupewa kadi nyekundu kwa changamoto hiyo, ingawa baadaye alitolewa nje baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano


"Haikuwa bure kwamba nilikuwa na hasira juu ya pambano hilo," alisema Ten Hag.


"Ilikuwa ni mchezo mbaya sana na jeraha baya. Nilidhani tulimpoteza kwa msimu mzima . Yuko mbele ya ratiba na tumefurahishwa sana na hilo," alisema


Ten Hag pia alithibitisha kuwa beki wa Uingereza Luke Shaw atakosa mchezo huo baada ya kuumia na kubadilishwa kipindi cha kwanza cha ushindi dhidi ya Brentford Jumatano


Ten Hag hakuthibitisha jeraha hilo lakini alisema ana uhakika Shaw atarejea hivi karibuni



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz