Napol yakubali kipigo Cha Mabao 4-0 dhidi ya Ac Millan - EDUSPORTSTZ

Latest

Napol yakubali kipigo Cha Mabao 4-0 dhidi ya Ac Millan

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Mabingwa watarajiwa wa Serie A Napoli jana walipata kichapo cha tatu msimu huu wakibomolewa mabao 4-0 na mabingwa watetezi AC Milan


Vijana wa Luciano Spalletti wanaendelea kuongoza ligi mbele ya Lazio walio nafasi ya pili kwa tofauti ya pointi 16, huku Milan wakipanda hadi nafasi ya tatu


Rafael Leao alifunga bao la kwanza na Brahim Diaz akaifungia Milan bao la pili. Leao akaweka la tatu kabla ya lexis Saelemaekers akafunga bao la nne


Timu hizo zitakutana tena katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa mwezi huu, tarehe 12 na 18 Aprili


Napoli, ambao wamekuwa bora msimu huu, sasa wamepoteza michezo miwili kati ya minne iliyopita ya Serie A, baada ya kuchapwa katika mechi moja kati ya 24 za kwanza


Lakini bado wanahitaji kushinda mechi tano kati ya 10 zilizosalia za ligi ili kujihakikishia ubingwa wa Serie A tangu 1990


Hiki kilikuwa kipigo chao kikubwa zaidi tangu kufungwa 5-1 na Atalanta mnamo 2007-08



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz