Matokeo Yanga vs kagera sugar leo - EDUSPORTSTZ

Latest

Matokeo Yanga vs kagera sugar leo

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Yanga inazidi kuukaribia ubingwa wa 29 Ligi Kuu ya NBC baada ya kuifumua Kagera Sugar mabao 5-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Azam Complex


Stephane Aziz Ki alikuwa shujaa wa Yanga katika mchezo huo akifunga mabao matatu 'hat-trik', mawili yakiwa mikwaju ya penati na moja likiwa bao la 'kideo' akiwa umbali takribani mita 25


Dhamira ya ushindi kwa Yanga ilionekana mapema kwenye kipindi cha kwanza, Fiston Mayele alikuwa na uchu wa kuongeza mabao yake


Alifanikiwa kufunga bao kwenye kipindi cha pili baada ya kosakosa nyingi katika kipindi cha kwanza


Bernard Morrison nae amerejea na bao lake, akiweka kambani bao la nne kwa shuti kali akiwa nje kidogo ya 18


Ilikuwa mechi ambayo Yanga walitawala na pengine walistahili kufunga zaidi ya mabao matano


Mayele amejiimarisha kileleni katika mbio za ufungaji bora akifikisha mabao 16, idadi sawa ya mabao ambayo alifunga msimu uliopita


Mabao yake matatu aliyofunga Aziz Ki leo, yamemfanya afikishe mabao nane msimu huu wakati Morrison amefunga bao lake la tatu leo


Yanga imerejesha gap la pointi nane dhidi ya watani zao Simba baada ya kufikisha alama 68 kileleni mwa msimamo wa ligi


Ushindi katika mchezo unaofuata dhidi ya Simba, utaihakikishia Yanga ubingwa kwani kimahesabu watahitaji alama mbili kutoka mechi nne zitakazokuwa zimesalia




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz