Kauli za makocha wa Simba kuelekea mechi ya kesho dhidi ya Ihefu Fc - EDUSPORTSTZ

Latest

Kauli za makocha wa Simba kuelekea mechi ya kesho dhidi ya Ihefu Fc

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Ihefu Fc ambao utapigwa Ijumaa, April 07 kwenye uwanja wa Azam Complex


Robertinho amesema anatambua mchezo huo hautakuwa mwepesi kwane wanakwenda kuchuana na timu iliyoimarika ambayo imetoa ushindani kwa timu zilizojuu kwenye msimamo wa ligi


"Hautakuwa mchezo rahisi lakini tunahitaji kucheza vizuri na kupata ushindi ili tusonge mbele hatua ya nusu fainali. Tunajua tunakwenda kukutana na timu ngumu lakini tumejipanga kuhakikisha tunashinda mchezo huo ili kutimiza malengo yetu," alisema Robertinho


Ihefu Fc tayari iko jijini Dar es salaam kuelekea mchezo huo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali


Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana kwenye ligi katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0


Baada ya mchezo wa kombe la FA, timu hizo zitaelekea Mbarali Mbeya kwa ajili ya mchezo wa duru ya pili ligi kuu ambapo utapigwa April 10 katika uwanja wa Highland Estates



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz