Hii hapa taarifa Mpya kuhusu Hassan Dilunga - EDUSPORTSTZ

Latest

Hii hapa taarifa Mpya kuhusu Hassan Dilunga

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amependekeza kurejeshwa kikosini kwa kiungo mshambuliaji Hassan Dilunga pale dirisha la usajili litakapofunguliwa


Mwaka mzima Dilunga alikuwa nje baada ya kuumia mazoezini, sasa ni miezi kadha imepita mchezaji huyo anafanya mazoezi na timu hiyo, jambo lililomshawishi Robertinho kukubali kiwango chake


Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zimebainisha kuwa Robertinho amewaambia viongozi kwamba ukianza usajili waanze na Dilunga anaona anamfaa kwenye kikosi chake


"Kwenye mazoezi Dilunga anaonyesha kiwango cha juu, kinachomfanya kocha aamini ni kati ya wazawa ambao wanaweza wakawa msaada mkubwa ndani ya kikosi chake msimu ujao"


"Dilunga aliumia akiwa na Simba, ndio maana alipewa nafasi ya kufanya mazoezi na wenzake, pamoja na hilo mchezaji mwenyewe hakujibweteka anapenda mazoezi na alionyesha ana kitu kikubwa kinachomfanya kocha apende kumuona kwenye kikosi chake na nafakiri ameshawaambia uongozi kuwa anamhitaji kwa ajili ya msimu ujao, kama watawezana basi ataonekana kwenye jezi ya Simba," alibainisha mtoa taarifa



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz