Alichokisema kocha wa Yanga kuelekea mechi ya kesho dhidi ya Rivers united - EDUSPORTSTZ

Latest

Alichokisema kocha wa Yanga kuelekea mechi ya kesho dhidi ya Rivers united

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kimekamilisha maandalizi kuelekea mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Rivers United


Mchezo huo utapigwa kesho Jumapili, April 30 katika uwanja wa Benjamin Mkapa


Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari, Nabi alisema hakuna jambo wanahitaji zaidi ya kupata ushindi dhidi ya Rivers United na kusonga mbele hatua ya nusu fainali


Nabi amesema ushindi waliopata Nigeria hautakuwa na maana kama watakosa ushindi katika mchezo wa kesho utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa


"Wachezaji wote wako vizuri, wanajituma sana mazoezini. Tunajua bado hatujafuzu, tunahitaji matokeo mazuri ili tusonge mbele hatua inaofuata"


"Nimekaa na wachezaji wangu, tumekubaliana kazi nzuri tuliyoifanya Nigeria itakuwa haina maana kama haitashinda mchezo wa kesho," alisema Nabi


Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, kiungo Zawadi Mauya amesema wanafahamu ushindi katika mchezo huo utawafanya waandike historia ya kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho kwa mara ya kwanza


"Tunajua tunakwenda katika mchezo ambao utaandika historia kwa klabu yetu. Lengo letu ni kuvuka ni kuvuka hapa na kufika mbali zaidi. Lakini kwa sasa tunaangalia mchezo uliopo mbele yetu tunahitaji ushindi tusonge mbele," alisema Mauya



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz