Yanga yawafumua waarabu yatinga robo fainali - EDUSPORTSTZ

Latest

Yanga yawafumua waarabu yatinga robo fainali

Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Yanga imetinga robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya US Monastir


Mabao ya Kennedy Musonda na Fiston Mayele yameihakikishia Yanga alama tatu muhimu ambazo sio tu zimewapeleka Wananchi robo fainali ya kombe la Shirikisho, Wananchi wamekaa kileleni mwa kundi D wakiwa na uwiano mzuri wa mabao kuliko Monastir


Ilikuwa mechi ambayo awali ilionekana kama ingekuwa ngumu kutokana na mazingira ya mvua kubwa kunyesha kwa saa kadhaa kabla ya mchezo


Hata hivyo wachezaji wa Yanga walipambana kuhakikisha wanautendea haki uwanja wa nyumbani na kuibuka na ushindi huo muhimu


Yanga imefikisha alama 10 ikiwa vinara wa kundi D sawa na Monastir


TP Mazembe wamepoteza mchezo dhidi ya Real Bamako kwa kuchapwa mabao 2-1 na hivyo kushushwa nafasi ya nne


Real Bamako wamepanda nafasi ya tatu wakiwa alama 5




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz