Vinara wa Mabao ligi ya Mabingwa Africa mpaka sasa - EDUSPORTSTZ

Latest

Vinara wa Mabao ligi ya Mabingwa Africa mpaka sasa

Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
 
Kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama yuko katika orodha ya vinara wa kuzifumania nyavu kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika


Chama alifunga hat-trik katika mchezo dhidi ya Horoya Ac uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa March 18 na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 7-0


Pia alifunga bao pekee la ushindi kwenye mchezo dhidi ya Vipers Fc uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa March 07


Katika hatua ya makundi Chama amepachika mabao manne na kutoa assist moja akiwa sawa na mshambuliaji Al Hilal Makabi Lilepo ambaye pia amefunga mabao manne na assit moja


Wachezaji wanaofuatia ambao wamefunga mabao matatu ni Hamza Khabba wa Raja Casablanca ya Morocco, Mahmoud Kahraba wa Al Ahly ya Misri, Cassius Mailula na Peter Shalulile wote wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambao kila mmoja ametupia mara tatu.


Chama alikuwa mchezaji bora wa wiki wa michuano hiyo baada ya mechi za raundi ya nne na ana nafasi kubwa ya kushinda tuzo hiyo baada ya mechi za raundi ya tano



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz