Tetesi za usajili barani ulaya Leo jumatano march 22 - EDUSPORTSTZ

Latest

Tetesi za usajili barani ulaya Leo jumatano march 22


 Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Manchester United imedhamiria kumnunua beki wa kati wa Monaco Axel Disasi, 25. (Mail)


Sheikh Jassim bin Hamad Al-Thani yuko tayari kuongeza ombi lake la kuinunua Manchester United kwa hadi £5.5bn. (The Mirror)


United na Liverpool wanaongoza Barcelona katika mbio za kumnunua kiungo wa kati wa Wolves na Ureno Ruben Neves, 26, msimu huu. (Football Insider)


Wachezaji wa Tottenham wamekuwa wakiwasiliana na meneja wa zamani Mauricio Pochettino kuhusu uwezekano wa kurejea katika klabu hiyo. (Sky Sports)


Mshambulizi wa Chelsea na Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 33, anaweza kurejea Barcelona kama chaguo la bei ya chini miezi 12 tu baada ya kuhamia Stamford Bridge. (Mundo Deportivo – In Spanish)


Chelsea wanaweza kumwachilia Aubameyang kutoka katika mkataba wake msimu huu wa joto. (Sport – In Spanish)


Paris St-Germain ndio klabu ya hivi punde zaidi kufikiria kumnunua mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24. (Foot Mercato – In French)


Real Madrid bado wako kwenye mazungumzo na kiungo wa kati wa Croatia Luka Modric kuhusu kandarasi mpya ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37, ambaye amezivutia klabu za Saudi Arabia na Qatar. (Sky Sports Germany)


Tottenham hawana uwezekano wa kutumia chaguo la kumsajili kwa mkopo mlinzi wa kati wa Ufaransa Clement Lenglet, 27, kutoka Barcelona kabisa. (AS – In Spanish)


Kiungo wa kati wa zamani wa Uingereza James Milner, 37, atalazimika kukatwa mshahara iwapo atatia saini mkataba mpya na Liverpool. (Football Insider)


Wamiliki wa Wolves wako kwenye mazungumzo ya kununua hisa katika klabu ya Ubelgiji ya K.V. Oostende. (Guardian)


Meneja wa zamani Harry Redknapp anasema angependa kufanya kazi na Ryan Mason ikiwa atakuwa meneja wa Tottenham kwa muda. (Sports)


BBC



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz