TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS - EDUSPORTSTZ

Latest

TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS

TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS

TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS

TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS

TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS

KAMATI ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetoa ruhusa kwa kiungo wa Yanga, Feisal Salum maarufu ‘Fei Toto’ kwenda kushitaki katika Mahakama ya Usuluhishi ya Masuala ya Soka ya Kimataifa (Cas).

Hiyo ni baada ya kamati hiyo, kutoa hukumu ya sakata lake la kuvunja mkataba wake wa miaka miwili alioubakisha Yanga.

Kamati hiyo, juzi Jumamosi ilitoa hukumu ya kiungo huyo kuwa inamtambua ni mali ya Yanga baada ya kupitia mikataba ya pande zote mbili.

Akizungumza na moja ya kituo cha Radio kikubwa hapa nchini, Mwenyikiti wa kamati hiyo, Said Sudi alisema kuwa Feisal ni mchezaji halali wa Yanga na baada ya kuupitia mkataba wake na kuonyesha wazi ni mali yao.

Sudi alisema kuwa wanatoa nafasi kwa kiungo huyo kwenda mbali zaidi na sio kurudi tena kwao TFF, ikiwemo CAS na wapo tayari kumpa review ili aende huko.

“Mkataba unaonyesha wazi ni mali ya Yanga, ila kama Feisal hajaridhika na maamuzi yetu anayo nafasi ya kukata rufaa na sisi tutampa review aende CAS sio hapa tena.

“Kwani hapa kwetu tayari hilo suala tumelimaliza, kwa kumuidhinisha ni mchezaji wa Yanga mwenye mkataba wa kuichezea timu yake hiyo,” alisema Sudi.

Aidha imefahamika kuwa Klabu ya Yanga SC na Mchezaji Feisal Salum Abdallah walishatumiwa nakala ya hukumu January 9, 2023 na hakuna mabadiliko yeyote kutoka taarifa ya awali kuwa Feisal ni mchezaji halali wa Klabu ya Yanga SC.

Nduruma Majembe ambaye ni wakili wa Feisal Kwa upande wa alisema: “Mteja wangu (Fei Toto) hana tena mapenzi ya kurudi na kuendelea kuitumikia klabu yake ya Yanga.

“Kwani katika kikao cha kamati aliweka dhahiri kwamba hakuna uwezekano wa yeye kurudi tena kuichezea Yanga. Labda atafutiwe mwanasaikolojia atakayebadilisha mawazo yake.

Wakiri huyo alisema kuwa licha ya kupokea nakala ya hukumu hawajaridhika na maamuzi ya TFF pia na mteja wake ambaye Ni Fei Toto hayupo tayari kurudi kuichezea timu ya Yanga hivyo wanajiandaa kwenda kushitaki katika mahaka ya usuruhishi wa michezo Duniani “CAS” na wanatarajia kufanya hivyo hivi karibuni

Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

DONWLOAD NIJUZE TV HAPA SISI kwetu Michezo ndiyo Furaha YETU.

Nipashe Michezo, Nijuze Michezo, Simba sc leo, Global Publishers michezo, saleh jembe michezo, Yanga leo, Shaffih dauda michezo, michezo, Magazeti, Usajili, Habari za Michezo, Nijuze Habari, Nijuze Michezo, Nijuze TV App, Nijuze TV LIVE, Nijuze Habari Michezo, Nijuze Habari Magazeti, Nijuze Habari Ajira, Nijuze Habari Usajili, Nijuze Habari Matokeo, Nijuze Habari Usajili, saleh jembe michezo leo,habari za michezo
leo 2023, habari za yanga za leo, habari za simba za leo, Habari za Michezo leo 2023.

The post TFF yamruhusu Feisal Kwenda CAS appeared first on Nijuze Mpya.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz