Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC - EDUSPORTSTZ

Latest

Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC

Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC

Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC

Clatous Chama Mchezaji Bora NBC Premier League December 2022, Juma Mgunda Kocha Bora NBC Premier League December 2022, Chama Mchezaji Bora NBC Premier League December 2022, Mgunda Kocha Bora NBC December 2022.

Clatous Chama Mchezaji Bora Ligi Kuu ya NBC, December 2022.

Clatous Chama Mchezaji Bora Ligi Kuu ya NBC, December 2022.

KIUNGO wa klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam, Clatous Chama amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi December wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2022/23, huku Kocha Mkuu wa timu hiyo Juma Mgunda akishinda tuzo ya Kocha Bora wa mwezi huo.

Kikao cha Kamati ya Tuzo za TFF kilichokutana Dar es Salaam Jumamosi ya January 7, 2023, kilimchagua Chama, baada ya kuonesha kiwango kizuri kwa mwezi December na kutoa mchango mkubwa kwa timu yake, ikiwa ni pamoja na kufunga mabao mawili na kuhusika na mengine matano katika michezo mitano aliyochezea timu hiyo.

Chama ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda John Bocco pia wa Simba na Fiston Mayele wa Yanga alioingia nao Fainali.

Juma Mgunda Kocha Bora Ligi Kuu ya NBC, December 2022.

Juma Mgunda Kocha Bora Ligi Kuu ya NBC, December 2022.

Kwa upande wa Mgunda yeye aliwashinda Nasreddine Nabi wa Yanga na Hans Pluijm wa Singida Big Stars alioingia nao Fainali.

Kwa Matokeo ya mwezi December Simba ilipanda kutoka nafasi ya tatu katika Msimamo wa Ligi ya NBC hadi ya pili.

Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC

Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC

Mgunda aliiongoza Simba katika michezo mitano, ikishinda minne na kutoka sare mmoja, ambapo Simba ilizifunga Coasta Union mabao 0-3, Geita Gold mabao 0- 5, KMC mabao 1-3 na Tanzania Prisons mabao 7-1huku ikitoka sare ya bao moja na Kagera Sugar.

Kwa upande wa Nabi kwa mwezi huo aliongoza Yanga katika michezo minne kati ya sita ambayo timu hiyo ilicheza na kushinda yote, ambapo Yanga ilizifunga Polisi Tanzania mabao 3-0, Coastal Union mabao 3-0, Azam FC mabao 2-3 na Mtibwa Sugar bao 0-1.

Michezo mingine ambayo Yanga ilishinda mwezi huo, lakini Nabi hakuiongoza kutokana na kutumikia adhabu ni dhidi ya Prisons ambayo Yanga ilishinda bao 1- O na dhidi ya Namungo ambayo Yanga ilishinda mabao 0-2.

Pluijm kwa mwezi December aliiongoza Singida katika michezo sita, akishinda minne, sare moja na kupoteza mmoja.

Singida ilizifunga Namungo FC mabao 3- 0, Tanzania Prisons mabao 1-2, Dodoma Jiji bao 0-1 na Geita Gold mabao 2-1, Ikitoka sare ya bao moja na Mbeya City na ilifungwa na Coastal Union mabao 1-2.

Godfrey Komba Meneja Bora wa Uwanja, December 2022. Uwanja wa Manungu, Morogoro.

Godfrey Komba Meneja Bora wa Uwanja, December 2022. Uwanja wa Manungu, Morogoro.

Pia Kamati ya Tuzo imemchagua Meneja wa Uwanja wa Manungu uliopo mkoani Morogoro, Godfrey Komba kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi December, kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.

Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

DONWLOAD NIJUZE TV HAPA SISI kwetu Michezo ndiyo Furaha YETU.

Nipashe Michezo, Nijuze Michezo, Simba sc leo, Global Publishers michezo, saleh jembe michezo, Yanga leo, Shaffih dauda michezo, michezo, Magazeti, Usajili, Habari za Michezo, Nijuze Habari, Nijuze Michezo, Nijuze TV App, Nijuze TV LIVE, Nijuze Habari Michezo, Nijuze Habari Magazeti, Nijuze Habari Ajira, Nijuze Habari Usajili, Nijuze Habari Matokeo, Nijuze Habari Usajili, saleh jembe michezo leo,habari za michezo
leo 2023, habari za yanga za leo, habari za simba za leo, Habari za Michezo leo 2023.

The post Chama, Mgunda watwaa tuzo Ligi Kuu ya NBC appeared first on Nijuze Mpya.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz