Diamond Platnumz Namba 4 Afrika...Afunguka Kuhusu Kifo Chake - EDUSPORTSTZ

Latest

Diamond Platnumz Namba 4 Afrika...Afunguka Kuhusu Kifo Chake


Supastaa Diamondplatnumz anaendelea kutunisha misuli Kimataifa akiiwakilisha vyema Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kwenye orodha ya wasanii 10 toka Afrika wenye ushawishi mkubwa ulimwenguni.


Jina la Diamond linashika namba 4 kwenye orodha hiyo ambapo nafasi nyingi zikitawaliwa na wasanii wa NIGERIA.


Aidha boss huyo wa WCB, kupitia insta story yake ame-share orodha hiyo na kueleza kwamba siku akiondoka duniani, basi bendera ya Tanzania itaacha kupepea kwenye anga la Kimataifa Kimuziki katika top 10, pengine labda top 100.


"Kiufupi ikitokea nimekufa 🇹🇿 haipo hapo. Pengine top 100 inshallah 🙏" - ameandika Diamond Platnumz.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz