LIVERPOOL YATINGA FAINALI LIGI YA MABINGWA -Michezoni leo - EDUSPORTSTZ

Latest

LIVERPOOL YATINGA FAINALI LIGI YA MABINGWA -Michezoni leo

Pakua App ya 'EDUSPORTSTZ NEWS' Uweze kufurahia Habari zote za Mapenzi; Udaku, Ajira na Michezo kila siku Ipo Google Playstore, Kwa Ku BONYEZA INSTALL Ili KUIDOWNLOAD Kwenye Simu yako nakutasoma habari zote hata kama hauna MB

LIVERPOOL imefanikiwa kwenda Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya wenyeji, Villarreal katika mchezo wa marudiano wa Robo Fainali usiku wa Jumanne Uwanja wa de la Cerámica mjini Villarreal nchini Hispania.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na Fabinho dakika ya 62, Luis Díaz dakika ya 67 na Sadio Mané dakika ya 74 baada ya Villarreal kutangulia kwa mabao ya Boulaye Dia dakika ya tatu na Francis Coquelin dakika ya 41.
Liverpool inafanikiwa kwenda Fainali kwa ushindi wa jumla wa 5-2 kufuatia ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza nyumbani, England wiki iliyopita.
Mechi ya mwisho ya marudiano ya Nusu Fainali ya UEFA Champions League inachezwa Jumatano usiku Hispania pia, baina ya wenyeji Real Madrid na Manchester City ya England Poa.
Mchezo wa kwanza Manchester City inayofundishwa na kocha Mspaniola, Pablo Franco Martin ilishinda 3-2 Uwanja wa Etihad.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz