Bei ya Mafuta yapanda Hadi Kiwango cha Juu zaidi Tangu 2008 - EDUSPORTSTZ

Latest

Bei ya Mafuta yapanda Hadi Kiwango cha Juu zaidi Tangu 2008



Bei ya mafuta imepanda hadi kiwango cha juu zaidi tangu 2008 baada ya Marekani kusema kuwa inajadili vikwazo vinavyowezekana kwa bidhaa za Urusi na washirika wake.

Brent crude - alama ya kimataifa ya mafuta - ilipanda hadi zaidi ya $139 kwa pipa, kabla ya kurudi chini hadi chini ya $130.

Masoko ya nishati yametikiswa katika siku za hivi karibuni kutokana na hofu ya usambazaji iliyosababishwa na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Wateja tayari wanahisi athari ya gharama ya juu ya nishati kadiri bei ya mafuta na bili za za majumbani zinavyoongezeka.


Masoko ya hisa barani Asia yalishuka siku ya Jumatatu, huku kampuni za Nikkei za Japan na Hang Seng huko Hong Kong zikishuka kwa zaidi ya 3%.

Siku ya Jumapili, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema utawala wa Biden na washirika wake wanajadili vikwazo vya usambazaji wa mafuta ya Urusi.

Baadaye, Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Nancy Pelosi alisema baraza hilo "linachunguza" sheria ya kupiga marufuku uagizaji wa mafuta ya Urusi na kwamba Bunge la Congress wiki hii lilinuia kupitisha msaada wa $10bn (£7.6bn) kwa Ukraine ili kukabiliana na uvamizi wa kijeshi wa Urusi.


"Kwa sasa Bunge linachunguza sheria dhabiti ambazo zitatenga zaidi Urusi kutoka kwa uchumi wa kimataifa," Bi Pelosi alisema katika barua.

Maoni hayo yametolewa huku shinikizo zikiongezeka kwa Ikulu ya White House na mataifa mengine ya Magharibi kuchukua hatua kali dhidi ya Moscow kutokana na uvamizi wake nchini Ukraine.

Vikwazo vya mafuta vya Urusi vitakuwa ongezeko kubwa katika kukabiliana na uvamizi wa Ukraine na kunaweza kuwa na athari kubwa kwa uchumi wa dunia.

"Wakati Marekani inaweza tu kusukuma marufuku ya uagizaji wa mafuta kutoka Urusi, Ulaya haiwezi kumudu kufanya hivyo. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba [kiongozi wa Urusi Vladimir] Putin, ikiwa atasukumwa ukutani, anaweza kuzima usambazaji wa gesi Ulaya, kukata njia ya nishati barani," Vandana Hari katika shirika la ushauri la masoko ya nishati Vanda Insights aliambia BBC.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz