Mwizi aiba chatu 15 wa kifalme Uingereza, msako mkali waanzishwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwizi aiba chatu 15 wa kifalme Uingereza, msako mkali waanzishwa




Msako Mkali Wanzishwa Baada ya Mwizi Kuiba Chatu 15 wa Kifalme Uingereza

Kulingana na polisi, chatu hao wa kifalme walichukuliwa kutoka katika eneo la Hillmorton eneo la Rugby siku ya Jumamosi, Disemba 11, asubuhi.

BBC inaripoti kuwa mwizi huyo anaaminika kuwachukuwa wanyama hao na kuwapakia baada ya kuingia kwenye nyumba iliyoko Horne Close, kabla ya kupitia kwenye makaburi yaliyo karibu na kutoroka.

Kando na nyoka hao, polisi wanasema kuwa funguo na pesa pia viliibwa.


 
Wapelelezi wanasema chatu hao wana alama za kibinafsi ambazo zitawafanya kutambulika kwa urahisi iwapo watapatikana.

Inaripotiwa kuwa mhalifu huyo aliwachukua viumbe hao kupitia makaburi ya Watts Lane kisha kukimbia nao.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz