Mwijaku Ampa Ushauri Zuchu "Yes mkamate kwa busara zitokazo kinywani mwako" - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwijaku Ampa Ushauri Zuchu "Yes mkamate kwa busara zitokazo kinywani mwako"


Moja kati ya headlines zinazo gonga vichwa vya habari mtandaoni ni issue inayomtaja mwanamuziki @diamondplatnumz kutaka kumuoa mwanamuziki mwenzake @officialzuchu , sakata ambalo kila mtu analizungumzia katika namna yake.

Sasa huenda sakata hili limemfikia mtangazaji kutoka clouds media, a.k.a. DC wa insta /maarufu kama msemaji wa maisha ya watu katika mitandao @mwijaku_01 baada ya kuandika ujumbe mrefu wenye mfano kutoka kwenye biblia ,ujumbe uliombatana na picha ya mwanamuziki Zuchu.

Katika post hiyo mwijaku alimaliza kwa kuandika maneno yanayo hisiwa kulenga sakata linalotajwa kuhusu #Diamondplatnumz kumuoa #Zuchu kwa kusema;

“Kuolewa na mtu sahihi sio kuomba tu, bali inaendana na uwezo wako wa kujitambua wewe binafsi, vipaumbele vyako visivyoathiri matakwa ya huyo mwanaume, kutambua mwanaume sahihi anapokuja kwako na kufahamu ni jinsi gani utamkamata kwa maneno matamu ya kinywa chako...Yes mkamate kwa busara zitokazo kinywani mwako!”✍@mwijaku_01

Je umeelewa alicho andika Mwijaku..!?






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz