Wafanyakazi wa Ndege Mashakani Baada ya Kuruhusu Abiria wa Ndege Kuuziwa Senene - EDUSPORTSTZ

Latest

Wafanyakazi wa Ndege Mashakani Baada ya Kuruhusu Abiria wa Ndege Kuuziwa Senene



Mwanamume asiyetambulika alionekana kwenye video akichuuza wadudu aina ya panzi kwa abiria walioukuwamo kwenye ndege ya Shirika la Uganda
Waziri wa kazi wa Uganda jenerali Katumba Wamala aliagiza shirika hilo la ndege, kuwachukulia hatua za kinidhamu wafanyakazi wa ndege waliomruhusu mtu huyo kuchuuza na kusababisha usumbufu

Panzi hao almaarufu Nsenene kwa Kiganda, wanapendwa kuliwa sana na raia wa Uganda na inasemekana kwamba huwa ni mlo mtamu
Video iliyozagaa mitandaoni ya mwanamume aliyekuwa akichuuza panzi ndani ya ndege ya shirika la Uganda kabla ya safari kung'oa nanga, imezua hisia mseto.

Video Yamwonyesha Mwanamume Akiwauzia Abiria Panzi Kwenye Ndege Kabla ya Safari
Mwanamume anatangamana na abiria waliokuwa ndani ya ndege wakielekea Dubai huku akiwauzia. Picha kwa hisani ya Sudhir.
Mwanamume huyo anaonekana akiwasisimua wateja walionunua panzi hao walikuwa wamewekwa ndani ya mifuko midogo ya plastiki.

Hata hivyo, habari ambazo hazijathibitishwa zinasema kwamba, wafanyakazi wa ndege hiyo waliachishwa kazi kwa muda baada ya kumruhusu mtu huyo kufanya uchuuzi ndani ya ndege. .

Kulingana na mwanahabari wa Ugand Sudhir Byaruhanga, wafanyakazi hao walilaumiwa kwa kumruhusu mchuuzi huyo ambaye hakuwa amevalia barakoa, kukiuka kanuni za kuzuia maambukizi ya kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya ugonjwa wa COVID-19.


Haya yanajiri baada ya Waziri wa Kazi wa Uganda Katumba Wamala kuagiza wafanyakazi waliokuwamo kwenye ndege hiyo kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa kile alichotaja kuwa ni ukosefu wa nidhamu.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz