Mwanamke aliyepanga kusafiri Saudia kwa ajili ya Umrah akamatwa akiwa na Cocaine Abuja - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwanamke aliyepanga kusafiri Saudia kwa ajili ya Umrah akamatwa akiwa na Cocaine Abuja



Shirika la kupambana na madawa ya kulevya nchini Nigeria (NDLEA) limesema kuwa limemkamata mwanamke aliyekuwa njiani kuelekea nchini Saudia kwa ajili ya Umrah akiwa na mifuko 80 ya cocaine katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Abuja.

Mshukiwa, huyo Adisa Afusat Olayinka, mzaliwa wa jimbo la Kwara, ambaye amekuwa akiishi eneo la Ibafo katika eneo la ​​Ogun, alikamatwa alipokuwa ndani ya Qatar Airways flight, imesema taarifa ya NDLEA, Jumatatu.

Mwanamke huyo amesema kuwa alianza kujihusisha na usafirishaji wa mihadarati baada ya kukutana na mwanamke mwingine katika Umrah katika mwaka 2019.

Hatahivyo, kulingana na taarifa, mwanamke huyo alisema alikuwa anataka kuchangisha Naira milioni 7 ili kuweza kutibiwa ili apate mtoto baada ya kuolewa kwa miaka 28 bila mtoto.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz