Diamond Platnumz Ajitoa Kwenye List ya Wasanii Wenye Account Chafu Instagram - EDUSPORTSTZ

Latest

Diamond Platnumz Ajitoa Kwenye List ya Wasanii Wenye Account Chafu Instagram



Moja kati wasanii wakubwa hapa Bongo ambao walikuwa ni wachafu wa account za Instagram ni pamoja na Diamond Platnumz. Ni msanii mkubwa Afrika mwenye idadi kubwa ya wafuasi kwenye mtandao wa Instagram lakini page yake hiyo ilikosa hadhi yenye kuendana na jina lake na ikawa yenye hadhi ya page za kina Carry Mastory ama local artists.

Iko wazi Diamond ana utajiri mkubwa wa mashabiki na fan pages za kutosha ambazo zinaweza fanya promotion ya hatari kwenye ishu zake,mbali na hapo ana ukurasa official wa kupost kazi zake ambao pia unaweza post challenges,kuna Tik Tok, lakini pia ana media ambazo zina uwezo mkubwa wa kusogeza kazi zake, alikuwa hana haja ya kupost mauchafu ambayo yanaharibu image ya acc yake kusudi tu ionekane ngoma inasumbua kitaa.

Kizuri Diamond ameacha kupost challenges kwenye ukurasa wake karibia project zake 3 za mwisho, lakini kibaya zaidi mashabiki zake wana yale mawazo ya hizo projects kuwa hajazifanyia promotion sababu wamezoeshwa kuona mauchafu hayo (video za challenges) kwenye ukurasa wake.

Si tu kuwa ameacha bali amefuta challenges nyingi kwenye ukurasa huo. Niliwahi andika hapa hapa kuwa anacho kifanya si cha hadhi yake na kwa hiyo akili kazidiwa hadi na mshindani wake Alikiba ambaye account yake ni safi muda mwingi, huku nikitoa mifano mingine ya mastaa kama Wizkid,Davido na Burna Boy namna walivyoachia page zao za habari zifanye kila kitu ila watumiaji wa bando bana wakacomment matusi.

Instagram ni moja ya taswira kubwa za celebrities,mfano juzi kati Diamond alipostiwa kwenye ukurasa wa WASHINGTON FC, mashabiki wa timu hiyo walikuwa hawamjui na suluhisho lilikuwa ni kukimbilia kutazama acc yake kuona ni nani hasa, wakiishia kushangazwa na uwingi wa followers alionao, imagine huyo anayechungulia acc anakutana na challenges kama mia ndio aje ajue huyu ni fulani keshajikatia tamaa hapo mwanzo tu,vipi ikiwa anakutana na show kama mia hivi,ni credit kubwa sana.

In short wasanii wetu inabidi wajue social media zao ni kwaajili ya Local Market au soko la nje.






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz