Chanzo Cha Ugomvi wa Square ni Mke wa Peter Inasemekana Mama Yao Alimkataa Kabla Hajafariki - EDUSPORTSTZ

Latest

Chanzo Cha Ugomvi wa Square ni Mke wa Peter Inasemekana Mama Yao Alimkataa Kabla Hajafariki


Inasemekana hivi sasa Paul(RudeBoy) na Peter(Mr.P) wanaelewana vizuri, tofauti zao wameziweka pembeni. Chanzo cha ugomvi wao kilikuwa ni Lola(mke wa peter)

Lola ni mdada wa mjini kwa nigeria na kwa story za mitandaoni hata mama yao P Square before hajafariki Hakua anakubali Lola awe na mwanawe, alisemaga hamtaki, kwanza kawazidi seven years hawa mapacha.

Pia Inasemekana huyu dada ni mjanja mjanja sana, sema ndio wanaume kichwa cha chini kikifanya basi cha juu kinastuck, hapo Peter akakomaa kumuoa huyo Lola.

Kundi la Psquare aliyekuwa anafanya lidumu ni bimkubwa wao, maana alivyofariki tu nafikiri hawakukaa hata miaka 2 vurugu zikaanza ila chanzo ni Lola kutaka Jude aache kuwasimamia psquare kwa kudai kuwa anawanyonya sana na wao ndo wanafanya kazi kubwa!

Paul aligoma kaka yao kuacha kuwa meneja wao lakini Peter akakaa upande wa mkewe (Lola) na hapo ndiyo shida ilipoanzia, wakatengana, wakarudiana, wakatengana tena na ndo hawakurudiana mpaka hivi sasa ndio wamelewana tena. Ila bado haijulikana kama watarudi kama kundi au vipi.

kwa mafanikio ya muziki, Rudeboy yuko juu...yule Peter mbwembwe tu then Paul(Rudeboy) ni mpole sana hana maneno maneno kama huyu Peter!





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz