Tanzia: Milionea Manga wa Gold Crest Afariki Dunia - EDUSPORTSTZ

Latest

Tanzia: Milionea Manga wa Gold Crest Afariki Dunia




Mfanyabiashara maarufu wa Madini na Kada wa Chama Cha Mapinduzi Jijini Arusha ambaye pia ni mmiliki wa Hotel za Gold Crest zilizopo Mwanza na Arusha, Mathias Manga amefariki dunia muda mfupi uliopita nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu.

Aliywahi kuwa Mbunge wa Shinyanga Mjini na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika, Stephen Masele ameandika kupitia akaunti yake ya Twitter….

“RIP Mathias Manga: Nimehuzunika sana. Siamini rafiki yangu umetangulia: Mtu mwema,mwenye roho nzuri na upendo, mkarimu, mwenye kujitoa kwa ajili ya jamii na watu. Mwenyezi Mungu akupe pumziko la amani. Pole kwa familia, ndugu na marafiki wote.”






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz