Maelfu ya watu wachomwa maji ya chumvi badala ya chanjo - EDUSPORTSTZ

Latest

Maelfu ya watu wachomwa maji ya chumvi badala ya chanjo



 
Maelfu ya watu wachomwa maji ya chumvi badala ya chanjo Ujerumani
Afisa mmoja anayefanya kazi katika kituo cha chanjo cha Schortens cha mkoa wa Friesland wa Lower Saxony, Ujerumani, aliitumia mchanganyiko wa maji ya chumvi badala ya chanjo ya corona (Kovid-19) kwa maelfu ya watu.

Gavana wa Friesland Sven Ambrosy alisema kuwa mnamo Machi na Aprili, ingawa hakuwa na hakika idadi kamili, takriban watu 9,650 walipewa maji ya chumvi badala ya chanjo za Biontech, Moderna na Astrazeneca.

Ilipogundulika kuwa afisa wa huduma ya afya aliingiza mchanganyiko wa maji ya chumvi badala ya chanjo ya Kovid-19, wale waliokuwa wamekumbwa na hali hiyo kati ya Machi 5 na Aprili 21 waliitwa kuchomwa chanjo tena.

Ilibainika kuwa ofisi ya mwendesha mashtaka inaendelea kuchunguza suala hilo.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz