- EDUSPORTSTZ

Latest

Hawa ndiyo wanyama watano ambao hufa baada ya kujamiana
Bongo5 · Hamza Fumo · 1 hour ago
Mambo ya kustaajabisha kuhusu wanyama, tumeangalia kwa ukaribu zaidi mpango wa uzalishaji unaofahamika kama Semelparity au kwa jina lingine uzazi wa kujitoa uhai, mara nyingi wanyama wengi huwekeza nguvu zao nyingi kwenye kuzaliana kabla ya kufa.




Panya mdogo aina ya antechinus wanaopatikana huko nchini Australia

Mmoja kati ya wanyama wa kipekee ni panya mdogo aina ya antechinus wanaopatikana huko nchini Australia, mnyama huyu mwenye sifa za kujamiana kwa muda wa saa 14, hali hii inapomtokea kinga ya mwili inaanza kudhoofu na hata kupelekea kifo chake.

Pengine unaweza kuita kujitoa mhanga kwa mzazi, Panya hawa aina ya ‘Antechinus’ hufariki katika mazingira hayo huku wakifahamu kuwa wameacha mbegu na kuzisambaza mbali zaidi.

“Jambo kubwa hapa ni kwamba spishi hizi zinapokutana huzaa watoto wengi zaidi,” Amesema Jeyaraney Kathirithamby, Mtaalamu wa entomolojia katika chuo kikuu cha Oxford.m

Upindukaji wa vimelea (parasites)
Kwa mfano, vimelea vyenye kutofautiana mfumo wa Strepsiptera, wanawake huzalisha kati ya mabuu 1,000 hadi 750,000 katika tendo lao moja walilokutana.

Wanyama hawa wana maisha ya kustaajabisha sana, wanyama wa kike huzika miili yao ndani ya mwili wa nyuki aliyekufa akijificha lakini huzingatia kutokuwa na mabawa, macho, miguu au antenna, huko pia uhifadhi vitoto vyake ambavyo huonekana kama peremende.


Sehemu pekee ya mwili wao ambayo hutoka kwenye mfereji wa mwili wa mdudu aliyekufa ndio hupitishia watoto, njia iliyowazi inamuwezesha mwanaume kupandikiza kwa wakike na mabuu kutoka nje. (Uhusiano: “Upendo wenye mahangaiko: Vimelea vya Kiume unavyowakamata wa kike shingoni kwa kutumia maumbile ya kiiume,”)

Nyuki wa kiume wanaoishi kwa saa nane, ambao huruka akiwa na nyuki jike na hujamiana mpaka kifo kinapowatenganisha, Kathirithamby anasema kwamba, Baada ya mabuu kutoka ndani ya mwili wa mwanamke naye pia hufa.

Maajabu mapenzi ya samaki
fish

Samaki huyu ni maarufu sana kwa kutotolesha mayai mengi sana.

Samaki wa kipasifiki hufa tu baada ya kuzaa-spishi wa chinook husifika kwa kutotolesha mayai mpaka 5,000.

Mikunga kutoka Amerika hutoa mayai mpaka milioni 30 kwa wakati muda mmoja, lakini maisha yao ya kuzalishana bado ni kimaajabu, anasema John Casselman, Mhadhiri wa chuo kikuu Ontario huko Canada.




Aina hii ya samaki huchukua miaka 20 kukua, mara nyingi maisha yao wanaenda mpaka ukingoni chini kabisa mwa bahari na hii inawapa maswali wataalamu kwani wameshindwa kufahamu wanavyozaliana, hata hivyo bado wanafanya uchunguzi wa kina zaidi kuona kama wataweza kupata njia zao.

Samaki huyu yuko hatarini zaidi kupotea kwa sababu nyingi zinazochangiwa na uvuvi wa kupita kiasi na ukarabati wa mabwawa makubwa, ndio maana ni vigumu kufahamu siri zao za kupandana.National Geographic

Buibui
Buibui wa kike, hupata hisia mbaya pale tu wadudu wengine hatari wa kike wanapoamua kula wenzi wao, lakini buibui aina ya Stegodyphus lineatus yeye huamua kufa kwa ajili ya watoto wake wasidhulike.



Baada ya kundi lake la kwanza la mayai kuanguliwa, “mama huchukua jukumu la kuwatafutia chakula buibui wadogo na kisha kuwaacha wamle yeye,” Amesema Catherine Scott, Mwanafunzi wa uzamivu katika chuo kikuu cha Toronto.

Buibui wa kiume huwa na tabia ya kujitolea miili yao ili tu waonekane kuwa wao ndi baba halisi wa buibui hao wadogo.

Buibui wa kiume “wana viungo viwili vya kuhamisha manii,ambavyo hufahamika kama pedipalps,” ambayo hutumia kuingizia mmoja baada ya nyingine kwenye sehemu ya buibui wa kike’ anasema Scott.

Baada ya kufa, “Mwili wa buibui wa kiume unasia katika nyeti za buibui wa kike na hii huwapa shida buibui wengine pale wanapopata matamanio ya kukutana na buibui huyo.

Buibui wa kiume aina ya Argiope hupendelea kukutana na wale walioteyari yeyuka na mwisho hushindwa kuwala. Lakini inapotokea ni buibui mzee , “Atamla baada tu ya kufa ,” Anasema Scott.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz