Dj wa Harmonize amtamani Alikiba - EDUSPORTSTZ

Latest

Dj wa Harmonize amtamani Alikiba

 


Official Dj wa msanii Harmonize Dj Seven Worldwide kutoka Konde Gang Music amefunguka kutamani kufanya kazi na msanii Alikiba anayewakilisha lebo ya Kings Music Records.

Dj Seven amesema haoni tofauti kufanya kazi na msanii mwingine nje ya Konde Gang kwa sababu mziki ni biashara na yeye anatafuta kitu kitakacholeta faida.

"Kuna msanii ambaye anamiliki lebo nimemuomba kufanya naye kazi kama itakuwa poa tutafanya, nataka kufanya kazi na Alikiba tumeshaongea na Producer wake Yogo kila kitu kikiwa sawa tutafanya wimbo" ameeleza Dj Seven Worldwide

Mpaka sasa Dj huyo ameshafanya kazi na wasanii mbalimbali wa BongoFlava kama Young Lunya, Salmin Swaggz, Linah, Mimi Mars na Baddest.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz