Picha chafu zilizomfanya P Mawenge kuachika - EDUSPORTSTZ

Latest

Picha chafu zilizomfanya P Mawenge kuachika

 


Rapa Positive Mawenge Kiwalani Kid amefunguka msala aliowahi kukutana nao kwenye mahusiano baada ya mwanamke mmoja kumtumia picha zisizokuwa na maadili wakati huo akiwa na mpenzi wake.

P Mawenge anasema kitendo hicho kilimfanya kuachwa na mpenzi wake huyo waliodumu kwenye mahusiano kwa kipindi cha miaka minne japo alijitahidi kujitetea lakini ikashindikana.

"Kuna mwanamke alinitumia picha WhatsApp sasa mpenzi wangu akaona picha za ajabu ajabu zinaingia iliniletea matatizo sana,  ni mtu ambaye tulikuwa tumezoeana mpaka mnazinguana halafu ile miyayusho inakuja kudondokea kwenye wakati usio rasmi au sahihi"

Aidha msanii huyo ameongeza kusema "Niliachika kwa sababu ya drama unajua ulimwengu wa sasa hivi una sababu nyingi sana za watu kugombana kwenye mahusiano na utandawazi ndio umeleta matatizo tofauti na zamani".





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz