Mzee Mpili "Tulipashwa Kuchukua Ubingwa wa Ligi Kuu, Sasa Mpira Kigoma" - EDUSPORTSTZ

Latest

Mzee Mpili "Tulipashwa Kuchukua Ubingwa wa Ligi Kuu, Sasa Mpira Kigoma"

 


 MZEE wa Yanga ambaye yupo kwenye baraza la Wazee, Mzee Mpili amesema kuwa kwa sasa wapo juu baada ya kuchukua pointi tatu na kituo kinachofuata ni Kigoma.

Yanga inatarajiwa kukutana na Simba kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho inayotarajiwa kuchezwa Julai 25, Uwanja wa Lake Tanganyika Kigoma.


Mpili ambaye alikuwa anatamba tangu awali kwamba Yanga itawafunga Simba ameweka wazi kwamba mpira Yanga upo na kituo kinachofuata ni Kigoma huko hawezi kuwaambia kwa sasa nini kitatokea.

"Matokeo tumeyapata na kama tumeomba matokeo tumepata basi tupo juu leo tumechukua pointi tatu tupo juu na pointi 70 na awali hesabu zetu ilikuwa kuchukua ubingwa.

"Watu wanaona mpira hatuna, sisi ilipaswa tuchukue ubingwa mwaka huu na unaona kwamba kwa sasa tupo juu. Watu ambao nipo nao ni sababu inayofanya tuwe tunajiamini hivyo tusubiri na tuone," amesema.

Yanga kwenye msimamo ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 70 baada ya kucheza mechi 32 Simba ipo nafasi ya kwanza na pointi zake ni 73 baada ya kucheza mechi 30.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz