Amkimbia Mbwana Ake Baada ya Kumfumania na CHUPI ya Mchepuko Mkononi - EDUSPORTSTZ

Latest

Amkimbia Mbwana Ake Baada ya Kumfumania na CHUPI ya Mchepuko Mkononi

 


Mwanamke mmoja kutoka Nguuni, eneo la Mwingi nchini Kenya  ameamua kumuacha mumewe baada ya kupata chupi ya mwanamke mwingine kwenye mfuko wa koti lake akifua nguo.

 Inasemekana kuwa jamaa alikuwa amerejea nyumbani siku iliyofuata mapema asubuhi akiwa mlevi chakari.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mrembo alimlaki mumewe na kumkaribisha nyumbani akamvua nguo chafu kisha akamtandikia kitanda alale ili stimu za pombe zimtoke mwilini.

 Inasemekana kwamba mzee alipokuwa akisukuma usingizi mkewe alianza kufua nguo na hapo ndiposa alipata chupi kutoka kwenye mfuko wa koti la mumewe.

Mama alipandwa na mori kutokana na kila alichokiona ambapo alifululiza hadi chumba alichokuwa amelala mumewe na kumwamsha kwa fujo.

“Wewe ulikesha kwa nani na chupi hii ni ya nani? Amka haraka wacha kujifanya hujui ninachokuuliza,” dada huyo alimcheka.

Jamaa aliropokwa kilevi bila kujua njama yake ya kuchepuka na wanawake wengine ilikuwa imefichuka baada ya chupi ya mpango wake wa kando kumsaliti ilipopatikana kwenye koti lake.

Hata hivyo, jamaa alikana chupi ilikuwa ya mpango wake wa kando. “Chupi gani hiyo? Chupi hiyo ni yako si ya mtu mwingine. Wacha kunilaumu bure,” jamaa alisema na kuendelea kulala.

Mwanamke huyo alimgutusha jamaa kwa kumzaba kofi usoni.

 “Amka haraka. Mimi sina chupi ya rangi hii. Wacha kujifanya eti hujui mwenyewe. Tabia yako imenifika kooni na sasa ninaondoka nikuachie mwenye chupi hiyo,” kisura alisema. 


Nafasi za Ajira Serikalini Bonyeza HAPA

Nafasi za Scholarships Bonyeza HAPA

 

Penyenye zinasema kwamba kipusa huyo alichukua kilichokuwa chake na kuondoka.

Inaarifiwa kwamba kimada wa jamaa aliweka chupi hiyo kwenye mfuko wa koti la jamaa kwa kusudi la kumkosanisha na mkewe.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz