Wafanyabiashara Kizimbani kwa Tuhuma za Kusafirisha Dawa za Kulevya zaidi ya Kilo Saba - EDUSPORTSTZ

Latest

Wafanyabiashara Kizimbani kwa Tuhuma za Kusafirisha Dawa za Kulevya zaidi ya Kilo Saba



WAFANYABIASHARA Abdallah Chande, mkazi wa Tegeta Ununio na Crispin Francis anayeishi Ununio Tegeta, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mawili ya kusafirisha dawa za kulevya zenye uzito wa zaidi ya kilo saba.

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa serikali Ester Martin mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Evodia Kyaruzi imedaiwa Juni 10,2021 huko Kimara Kilungure katika Manispaa ya Ubungo mkoani Dar es Salaam, washtakiwa wakutwa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine zenye uzito wa kilo 7. Na gramu 73.

Aidha mshtakiwa Francis anadaiwa siku hiyo akiwa eneo la Kinondoni Manyanya alipatikana akisafirsha dawa za kulevya aina ya bangi zenye uzito wa gramu 2.94.

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi ambazo kwa kawaida husikilizwa mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi Julia 8,mwaka huu.





Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz