Rais Museveni Atangaza Masharti Mapya Kupambana na Covid- 19 - EDUSPORTSTZ

Latest

Rais Museveni Atangaza Masharti Mapya Kupambana na Covid- 19




RAIS wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza   masharti mapya ya kupambana na ongezeko la visa vya virusi vya Corona nchini humo, Hatua hizo zilianza kutekelezwa saa 10:00 jioni,  jana Juni 18.

 

Kwenye hotuba iliyorushwa kupitia runinga Ijumaa  usiku Juni 18, Museveni alitangaza kuwa usafiri wote wa kibinafsi na wa umma nchini umepigwa marufuku kwa siku 42 zijazo isipokuwa kwa huduma muhimu na mizigo.

 

Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Entebbe na vivuko vingine vya mpaka wa ardhi hata hivyo vitabaki wazi kwa watalii na wale wanaorejea lakini mamlaka zimepewa jukumu la kuhakikisha kuwa hakuna kesi chanya au aina mpya za covid zinazoingia nchini humo

.

Amri ya kutotoka nje imesongeshwa kutoka saa tatu usiku hadi saa moja usiku na itadumu hadi saa kumi na moja unusu alfajiri .Waendeshaji pikipiki, wanaojulikana kama Boda Boda wanaruhusiwa kubeba bidhaa tu.

 

Kazi zote zinazozingatiwa sio za lazima, shule na taasisi za kujifunzia, sehemu za ibada, na hafla za michezo pia zimefungwa kwa siku 42 zijazo.

Vituo vya biashara na maeneo ya biashara pia yamefungwa na wachuuzi wa soko wakiruhusiwa kulala kwenye vibanda vyao.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz