DEAR LADIES Ni jukumu lako kuwa romantic kwa mumeo. Aibu yako isikuzuie kuonyesha mapenzi yako kwa mume wako. - EDUSPORTSTZ

Latest

DEAR LADIES Ni jukumu lako kuwa romantic kwa mumeo. Aibu yako isikuzuie kuonyesha mapenzi yako kwa mume wako.

 BIG : phatbootycuties

Mtumie meseji mume wako anapokuwa kazini, muda mwingine hata kama yupo nyumbani mnaangalia TV chati nae katika mitandao ya kijamii (watsapp, Facebook etc) hata kama yupo mbele yako.
Hii huleta faraja na ni njia mojawapo ya kuwa romantic kwa mwanaume wako. Jadiliana nae jinsi gani anavyokuvutia. Mnunulie zawadi hata leso, boxer, tai, viatu nk. Mnapokua mezani mkila pamoja labda nyama, mpe nyama kubwa kuliko zote.
Kama muda unao mtengenezee keki na juice ya matunda na msuprise nayo. Wadada, tumieni sauti yenu laini kumbembeleza na kumdekea, muimbie mnapokua pamoja chumbani, acheni userious kama mpo kwenye kikao cha bodi ya Korosho.
Mume wako anaporudi toka kazini usimkaribishe huku umenuna utafikiri shabiki wa Arsenal aliekosa kombe baada ya msimu wa ligi kuisha. Usimkaribishe mume wako huku mwili wako ukinukia mchuzi wa samaki au pilipili hoho, kuwa msafi na unukie. Wanaume hawapendi mwanamke mchafu
Mkaribishe kwa kumkumbatia kila siku, na asubuhi anapoenda kazini Muombee Mungu amwepushe na mabalaa na muombee mafanikio. Msupport, mshauri, muondoe uchungu, mfariji pale panapokua na matatizo, sio kazi ndogo kuwa mwanaume.

Pale unapoona anapoteza matumaini ni kazi yako kumpa moyo ni wakati ambao anakuhitaji sana uwe karibu yake na sio kumkwaza tena. Usimfananishe na wanaume wengine. Mpikie chakula akipendacho, mfulie nguo zake, osha gari lake, mvalishe nguo na mpeti peti akiwa anaumwa.
Muamshe asubuhi na mapema, na usimlalamikie kama ana tabia ya kukoroma. Acha Kiss iwe njia yenu ya kuwasiliana. Mpe kitu inaitwa Morning glory (tendo la ndoa la asubuhi), hakikisha unamkamua vilivyo ili asitizame wanawake wengine pembeni! Soma vitabu kuelewa namna ya kuishi na mume, usijifunze kutoka katika movie. Ya kwenye Muvi Mengi sio ya kweli.
Muite mume wako jina lake la utani pia muite jina lake halisi hata kama ni mkubwa sana kuliko wewe as far as he is comfortable with it.
Msupport katika hobby zake, kama anapenda mpira jikite kuijua timu anayoishabikia, mnunulie jezi ya hiyo timu, kama mna watoto wananulie jezi ya timu anayoipenda baba yao na wavalishe. Usinune anavoenda kuangalia mpira. Mpira ni starehe kubwa sana kwa wanaume na huwafanya watengeneze marafiki kila siku
Kumbuka Mwenyezi Mungu ameagiza wanawake kuwatii wanaume zao, hivyo basi mheshimu na kumtii hata kama ni mdogo kuliko wewe. Ndoa sio show off bali ni kujitoa kwa moyo wote. Hakuna jambo zuri kwa watu wawili wanaopendana kweli zaidi ya Ndoa na ukiona Mwanaume anasua sua kila ukimueleza suala la Ndoa, ujue huyo hayuko serious.
Na mwanaume ukipata mwanamke wa aina hii ni kwa nini uhangaike na michepuko iliyojaa laana ambayo ni mawakala wa shetani katika kuvunja taasisi imara ya ndoa iliyoundwa na Mungu mwenyewe?


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz