Madhara Kwa Mwanamke/Mwanaume Waliofanya Mapenzi Wakati wa Hedhi - EDUSPORTSTZ

Latest

Madhara Kwa Mwanamke/Mwanaume Waliofanya Mapenzi Wakati wa Hedhi

Madhara Kwa Mwanamke/Mwanaume Waliofanya Mapenzi Wakati wa Hedhi

Kwa mujibu wa wataalamu wametoa maelezo mafupi juu ya maana sahihi ya hedhi na kusema kuwa ni kipindi maalumu katika mzunguko wa mwanamke mwenye umri wa kuzaa. Wakati huo, ambao kwa kawaida unarudi kila baada ya mwezi mmoja kwa kutokwa na damu kwenye uke.

Ni vyema kufahamu mambo kadhaa hasa yanayohusu masuala ya afya ambayo muda mwingine tunaweza kuwa tunayafanya bila kutambua madhara yake.

Madaktari katika tafiti zao walichambua baadhi ya madhara kwa mwanamke na mwanaume kushiriki tendo wakati wa hedhi.

Ambapo kwa upande wa mwanaume takribani madhara 6 yaliweza kuainishwa yakiwemo.

Kupata maambukizi katika njia ya mkojo hadi kwenye kibofu

Maambukizi katika tezi dume, hii inaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanaume.

Kuziba kwa njia ya mkojo

Utasa au ugumba

Ulegevu wa misuli ya uume na upungufu wa nguvu za kiume

Athari mbaya ya kisaikolojia kwa kufanya tendo katika mazingira yasiyo safi hali inayoweza kupelekea kutolifurahia.

Lakini pia madaktari hao waliweza kuainisha athari za kushiriki tendo kwa mwanamke aliye mwezini.

Kupata maambukizi katika viungo vya ndani vya uzazi kama vile shingo ya kizazi, mirija ya uzazi kwa ujumla anaweza kupata matatizo na kuathiri mfumo wake wa uzazi

Maumivu makali ya tumbo hasa kwa wale wanaopatwa na maumivu wakati wa hedhi

Utokali damu unaweza ukaongezeka kuliko vile inavyotoka kwa kawaida

Utasa au Ugumba

Kuvimba kwa kuta za ndani za uke kwa kuwa wakati wa hedhi zenyewe huwa tayari zimevimba kweney uke wakati wa tendo

Mwanamke hiathirika kisaikolojia n akutokufarahia tendo.


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz