TATIZO LA KICHOMI NI MOJA YA DALILI ZA UGONJWA MOYO� - EDUSPORTSTZ

Latest

TATIZO LA KICHOMI NI MOJA YA DALILI ZA UGONJWA MOYO�


UTAMUZAIDIAPP
VIJANA wengi leo nyumbani Bongo wanapatwa na maradhi ambayo zamani yalikuwa ya wazee
au watu wa makamo. Maradhi haya ni kama kisukari na mstuko wa moyo.
Kichomi ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya.
Ukipatwa muda mrefu au kila wakti ; basi �chunguza zaidi.
Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa.
1.
Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi
Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic
Jambo la kuangalia ni je?
1.
Unashikwa kichomi ukiwa unatembea?
Umeinama au umelala
Ukishakula chakula
Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo.
Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa
wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng�enyui sawasawa linachoka.
Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo.
Tatizo jingine ni ulaji wa chakula chenye chumvi nyingi sana. Chumvi inakorofisha pia mzunguko wa damu mwilini.
Hasa kama hunywi maji.
Kunywa sana Maji ya Uvuguvugu yatakusaidia kuondowa tatizo la kichumi.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz