RAFIKI YAKO ANAPOKWAMBIA NDOA NI UVUMILIVU KWAMBA HATA YEYE ANAVUMILIA HEBU JIULIZE ANAVUMILIA NINI NA KWA SABABU GANI? - EDUSPORTSTZ

Latest

RAFIKI YAKO ANAPOKWAMBIA NDOA NI UVUMILIVU KWAMBA HATA YEYE ANAVUMILIA HEBU JIULIZE ANAVUMILIA NINI NA KWA SABABU GANI?



COMMON MISTAKES OF MEN IN MARRIAGE/RELATIONSHIP - Ufundi Chumbani
Kuna mtu anavumilia kwasababu hana kazi na siku akipata basi anaondoka.
Kuna mtu anavumilia kwakuwa kazi anayoifanya haimpi aina ya maisha ambayo anayataka hivyo analazimika kuvumilia ili aendelee kuishi vizuri.
Kuna mtu anavumilia kwakuwa anajua sababu ya kumpata huyo mwanaume/mwanamke labda aliroga sana na sasa anachokipata ni matunda yake.
Lakini kuna mtu anavumilia kwakuwa kama ni magonjwa kashaambukizwa hivyo anaona kuwa hata akiondoka hakuna kipya huko nje, lakini kuna mtu anavumilia kwakuwa moyo wake ushakufa ganzi hahisi tena maumivu ashajikatia tamaa na maisha yake.
Kwa maana hiyo, usidanganywe na tabasamu lake la nje pale anapokwambia vumilia, bali angalia anavumilia kwa sababu gani na wewe jiulize unataka uvumilie kwa sababu gani?
Je ni kwamba umeizoea hiyo hali ya matesozmaumivu,dharau na hutaki tena mabadiliko? Je kuna matumaini kuwa kutakuwa na mabadiliko mbeleni?
Je, huna pakwenda na kila mtu anakuona mzigo? Je, umeshachoka maisha na huna mpango wa furaha tena? Je, kashakuambukiza kila ugonjwa na hakuna jipya la kukupa?
Ndiyo acha tu kuvumilia kwakuwa kila mtu anavumilia, wewe si kila mtu, wewe si wao, maumivu yako si yao na wala maumivu yao si yako.
Ni lazima ujifunze kufanya mambo kwa ajili yako na si kufanya mambo kwa kuwa kila mtu anafanya tumeelewana hapo sawa sawa?.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz