PITIA HAPA KIDOGO. SAIKOLOJIA INASEMA NINI JUU YA MAHUSIANO. - EDUSPORTSTZ

Latest

PITIA HAPA KIDOGO. SAIKOLOJIA INASEMA NINI JUU YA MAHUSIANO.


1.Saikolojia inasema,kitu kichoumiza zaidi juu ya usaliati ni kwamba haufanywi na adui bali ni wale unaowaamini zaidi kuliko wengine.
2. Wapenzi au wachumba wanaotumia angalau dakika 10 ndani ya siku moja kufurahi pamoja inaelekea wakawa na uhusiano imara na mapenzi yakadumu.
Jiulize wewe ulifurahi lini mara ya mwisho?
3. Ukiwa na mchumba/mpenzi ambaye anakufanya kila siku uumie na anasumbua ktk maisha, kamwe usijaribu kumbadilisha achana nae ktk maisha yako, kwani ipo siku atasema ulinitaka mwenyewe kuning'ang'ania!
4.Saikolijia inafundisha kuwa watu wengi hawapendi majibu ya mkatao hasa katika mahusiano, na jibu "K" ndio hukera zaidi,yaani mtu anaongea maneno mengi alafu mwenzako anajibu herufi moja tu, k.
5.Saikolojia inasema kuwa wanaume huwa wanasahau lakini kamwe hawasamehe,wanawake wanasamehe lakini kamwe hawsahau.
6. ukweli ni kuwa watu wanao ficha hisia zao na kutoonyesha wivu ndio hujali zaidii katika mapenzi, na huumia zaidi pindi uhusiano unapoisha au kuvunjika.
ZINGATIA HAYA
1. Kamwe usimkatae mtu anayekujali na kukupenda kwa dhati kisa wapita njia,ipo siku utagundua umepoteza mwezi na wakati huo utakuwa ukihesabu nyota na kuchomwa moyoni.
2. Watu au marafiki hawatakuwa waamuzi wakubwa siku zote ktk maisha yako,watashauri ila mwamuzi wa mwisho ni wewe.
Jifunze kuamua mambo mwenyewe.
3. Kamwe usikate tamaa kisa mamboa magumu,wengi walianza katika kipindi kigumu kama chako na mapito yao huenda yalikuwa mmagumu kuliko hata yako.
Kama makalio tu kwa mwanadamu,yapo madogo na makubwa.
4.Huwezi ishi maisha ya kuumia kwa ajili ya asiyeumia juu yako,
fanya kilicho halali juu yako hata kama kitaumiza,tengeneza furaha ya kudumu.
5. Furaha ya kweli ni yakutoka moyoni,si kuwa na mali kwani mali zaweza toweka wakati wowote ukakosa furaha.
6. Marafiki wazuri ni wale amabao huchukaua tatizo lako kama lao husaidia na hivo kama una marafiki hawatakuacha uteseke ukiwa na tatizo ila watakusaidia.
7. Kamwe usiruhusu moyo wako umfanye mtu awe kila kitu moyoni mwaka/kwako wakati yeye kakufanya wa ziada katika moyo wake.
8. Ni bora kueleza hisia zako kwa unaempenda,kukaa kimya sio dhahabu utapoteza mtu wa msingi kisa kukaa kimya, funguka kijana,dada eleza ya moyoni usiogope.
MAPENZI kitu kizuri sanaa ila yanatesa na kuumiza moyo,yakichanganya ni mataaam,ilaaaaa sasa,usiombe.
Ahsante




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz