KWA NINI UNASHINDWA KUJUA SIKU ZAKO ZA UZAZI, HATARI NA SALAMA? - EDUSPORTSTZ

Latest

KWA NINI UNASHINDWA KUJUA SIKU ZAKO ZA UZAZI, HATARI NA SALAMA?


1- Ni kwa sababu ya kupata elimu ya mtaani ambayo ni ya jumla sana na ambayo ina maelezo kana kwamba kila mwanamke ana mzunguko sawa na mwingine na kwamba hautaweza badilika hata kama ukiumwa au ukipata masaibu makubwa ya msiba.
2- Ni kwa sababu umepata elimu ya darasani au vitabuni bila kufuatilia kwa makini sana uhalisia wa mzunguko wako wa hedhi na upatikanaji wa mimba
3- Ni kwa sababu huna mtu/mwalimu mwenye uzoefu wa kutosha kuweza kukufundisha vizuri na kufuatilia mzunguko wako wa hedhi na uhalisia wa dalili zako za siku za uzazi.
KUNA AINA TATU ZA MIZUNGUKO YA HEDHI
#WAKWANZA - mzunguko kamili, huu ni mzunguko wa hedhi usioyumba na haubadiliki (labda kutokee matukio makubwa ya kimaisha) mfano mtu kila mwezi anaingia tarehe 3 kwenye bleed, au kila mwezi anarudi nyuma siku 3 au kila mwezi anaongeza siku 2 mbele. HUU NI MZUNGUKO KAMILI
mfano wa mwanne mawazo
mwezi wa saba anamzunguko wa hedhi wa siku 28
mwezi wa nane anamzunguko wa hedhi wa siku 28
mwezi wa tisa anamzunguko wa hedhi wa siku 28
#WAPILI - mzunguko unaoyumba kidogo (kati ya siku 1 - hadi 4). Mzunguko huu ni ule unaoyumba kidogo lakini hauyumbi sana.
Mfano wa Asha wa Makoroboi
mwezi wa 7 alikuwa na mzunguko wa hedhi wa siku 25,
mwezi wa nane akawa na mzunguko wa hedhi wasiku 28
na mwezi wa tisa akawa na mzunguko wa hedhi wa siku 24.
Ukiangalia hapa utaona ya kwamba huu sio mzunguko kamili kama ule wa aina ya kwanza lakini ni mzunguko unaoyumba kidogo kati ya siku 1-4...
#WATATU - mzunguko unaoyumba sana lakini myumbo wake upo kati ya siku 21 hadi 35. Huu ni mzunguko unaoyumba zaidi ya siku 4 lakini chini ya siku 15.
Mfano wa Anna wa mhogo.
Yeye alikuwa na mzunguko wa hedhi ifuatayo kwa mwezi wa saba, nane na tisa
mwezi wa saba mzunguko wake wa hedhi wa siku 21
mwezi wa nane mzunguko wakewa hedhi wa siku 30
mwezi wa tisa mzunguko wake wa hedhi wa siku 33
ukiangalia kwa makini utakuta ya kwamba mzunguko huu kila mwezi uko tofauti na mwingine, lakini unazidi tofauti ya siku zaidi ya 4 lakini sio zaidi ya siku 15
AINA YA NNE NA MWISHO NI MZUNGUKO VURUGU
Huu ni mzunguko wa hedhi usiojulikana kabisa, na ambao unaweza kuwa na mzunguko wa chini ya siku 21 au zaidi ya siku 35. na miezi mingine mtu anaenda hadi siku 60 hajapata hedhi. Hili ni tatizo kabisa na cha kwanza lazima ufike hospitalini kujua nini shida yako ndio uweze kusadiwa.....
Katika hizo aina 3 za kwanza za mizunguko unaweza kuwa na mzunguko wa hedhi mfupi (siku 21-25)
mzunguko wa hedhi wa kawaida (siku 26-30)
au mzunguko wa hedhi mrefu (siku 31-35).
Point hii ni muhimu sana hasa kwa wenye mizunguko mifupi kwa kuwa ili uweze kupata mimba basi inakufaa ukisha maliza bleed tu siku zako za uzazi zinaanza, kwa hiyo unashauriwa uanze tendo la ndoa,
WENGINE PIA HUSHAURIWA WAFANYE TENDO LA NDOA KATIKA SIKU ZA BLEED KITU AMBACHO SIYO KIZURI...
Kwa elimu ya afya, ushauri na tiba....
share wapate wenzako pia
UTAMUZAIDIAPP




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz