*JINSI YA KUMSAHAU MPENZI WA ZAMANI KIRAHISI ZAIDI* - EDUSPORTSTZ

Latest

*JINSI YA KUMSAHAU MPENZI WA ZAMANI KIRAHISI ZAIDI*

_You chucked me, now leave me alone: Fading Zari blasts former ...

*Mahusiano ni sehemu kubwa sana katika kufanikiwa au kutokufanikiwa kwenye maisha yako, kama hauko kwenye mahusiano mazuri unaweza kukuta ndoto zako zinakufa na unashindwa kuwa yule mtu ambae umepanga kuwa kwenye maisha yako, lakini pia kama ukiweza kuyatumia mahusiano vizuri pia yanaweza kuwa sehemu ya kufanikiwa kwenye maisha yako.*_ _*Watu wengi sana hasa vijana wako kwenye mahusiano yasiokuwa na tija, lakini wanashindwa kujinasua huko kwa kuogopa kuumia au kumuumiza mwenzake, na ni kweli unajua muda fulani kwenye maisha unaweza kuwa na mtu ambae umemzoea kabisa anakufanyia mambo ambayo yanakurudisha nyuma lakini unashindwa kumuacha kwasababu unaogopa maumivu.*_ _*Leo nitakufundisha jinsi ya kumuacha mpenzi wako ambae hana tija kwenye maisha yako bila kumsababishia maumivu.*_ _*Yawezekana upo katika Mahusiano ya

siyo na tija kwako na unashindwa kuvunja mahusiano hayo.*_ *Tumia njia zifuatazo kuvunja uhusiano huo:-* *1. PUNGUZA MAWASILIANO NAE.* _*Njia ya kwanza kabisa ya kuacha mahusiano yasio na tija bila kusababisha maumivu ni kupunguza mawasiliano, kama mlikuwa mnawasiliana mara tano kwa siku anza kufanya mara tatu kwa siku, baada ya muda fanya mara mbili, baadae tena mara moja, najua utapokea maswali mengi mara ooh mbona siku hizi hunipigiii jibu rahisi tu niko busy au sina vocha, mwisho wa siku atazoea.*_

 *2. PUNGUZA MUDA WA KUKUTANA NAE.* _*Kama mlikuwa mnaonana mara mbili kwa wiki anza kumpa nafasi ya kuonana mara moja kwa wiki, halafu ongeza kazi za kufanya ili hata akisema akutafute yeye atakukuta tu uko kwenye kazi nyingine najua utapokea maswali mengi sana, cha msingi ongea naye vizuri mwambie kuna majukumu yameongezeka, mwanzo itakuwa ngumu lakini mwisho wa siku atazoea tu.*_ _*wewe umeshaona kuwa hayo mahusiano hayakufikishi kwenye ndoto zako.*_ 

*3. FANYA MAZOEZI SANA.* _*Kama ulikuwa huna tabia ya kufanya mazoezi ya viungo anza kufanya mazoezi ya viungo, mazoezi yanakufanya uwe busy muda mwingi na yanakuondolea mawazo yote, hii itakufanya uwe mtulivu sana siku zote.*_ 

*4. PUNGUZA MATUMIZI KWAKE NA ANZA KUWEKA AKIBA.* _*Hapa inabidi uwe mtu wa sina hela, punguza kabisa matumizi kwake halafu anza kuweka akiba, kama ulikuwa unamfanyia manunuzi mara kwa mara punguza halafu weka akiba, ili ikusaidie baadae.*_ 

*5. MFANYE AWE RAFIKI YAKO.* _*Ukitaka kuachana na mahusiano yasio na tija haina haja ya kumfanyia visa mwenzako, au kumuonyeshea kuwa humtaki tena hapana inaweza kukuumiza wewe zaidi au ikamuumiza yeye zaidi, maisha siku zote hayaeleweki, unaweza kuona leo mtu hana msaada kwako lakini siku nyingine akawa msaada kwako, sasa msiachane vibaya hata kama umegundua kuwa mahusiano hayo hayakufikishi kwenye ndoto zako, cha msingi wewe mfanye awe rafiki yako, tena ikiwezekana kama ulikuwa unamuita majina ya kimapenzi muda wote anza kumuita rafiki.*_ _*Itakuwa ngumu mwanzo lakini atazoea tu.*_ 


*6. ANZA KUMSHAURI SANA KUHUSU MAISHA KULIKO MAPENZI.* _*Tumia muda wako mwingi kila mnapokutana kuzungumzia maisha na ndoto zenu, mshauri sana kuhusu maisha kuliko mapenzi utaona kuna nguvu fulani hivi ambayo ilikuwa imezoeleka itaanza kupungua siku hadi siku na mwisho wa siku mnaachana kirafiki kabisa na kila mtu anaendelea na maisha yake huku mkiwa mnaongea kama kawaida.*_ _*Kwenye maisha usikubali kabisa mahusiano yavuruge ndoto zako na malengo yako ya kimaisha, ukiona tu uko kwenye mahusiano ambayo unaona yanapokupelekea ni kupoteza ndoto zako anza kuyaacha mapema sana.*_



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz